.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 11 Mei 2017

ALEXIS SANCHEZ NA OLIVIER GIROUD WAIPANDISHA ARSENAL NAFASI YA TANO

Timu ya Arsenal imezidi kuweka hai matumaini yake ya kumaliza katika nafasi za nne za juu za Ligi Kuu ya Uingereza baada ya kufunga magoli mawili katika kipindi cha pili yaliyofungwa na Alexis Sanchez na Olivier Giroud na kuibuka na ushindi wa 2-0 dhidi ya Southampton.

Katika mchezo huo wa jana kipindi cha kwanza hakikuwa na soka la kuvutia na kiliisha bila nyavu kutikiswa, lakini kilipoanza kipindi cha pili alikuwa Sanchez aliyeanza kutikisa nyavu kwa kuwahadaa mabeki wawili na kuutumbukiza mpira kimiani.

Giroud aliyekuwa akitokea benchi kwa aliipatia Arsenal goli la pili kwa mpira wa kichwa cha karibu na goli, dakika chache tu tangu aingie dimbani.
                       Alexis Sanchez akiifungia Arsenal goli la kwanza katika mchezo huo 
                 Olivier Giroud akiruga juu na kuupiga kwa kichwa mpira na kufunga goli

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni