.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 11 Mei 2017

REAL MADRID YAIFUATA JUVENTUS FAINALI YA LIGI YA MABINGWA ULAYA

Mabingwa watetezi wa Ligi ya Mabingwa Ulaya, Real Madrid, wametinga fainali na sasa watavaana na Juventus katika dimba la Cardiff, baada ya kuwatoa majirani zao Atletico Madrid.

Atletico, iliyokuwa nyuma kwa magoli 3-0 katika mchezo wa kwanza, ilianza kwa kishindo mchezo wa jana na kuongoza kwa magoli 2-0 kupitia kwa Saul Niguez na Antoine Griezmann kwa mkaju wa penati.

Hata hivyo Real Madrid walipata goli pale Isco alipounasa mpira uliorudi baada ya shuti kali la Toni Kroos kutemwa, kufuatia nafasi nzuri aliyotengeneza Karim Benzema kwa kutoka mbio vyema lakini mpira ukaokolewa.
                    Saul Niguez akiruga juu na kuupiga mpira kwa kichwa uliojaa wavuni
                                    Antoine Griezmann akifunga kiufundi mkwaju wa penati
                    Isco akiuwahi mpira na kufunga goli pekee la Real Madrid hapo jana

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni