.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 12 Mei 2017

JAMBAZI MREMBO AUWAWA KWA KUPIGWA RISASI NA POLISI KENYA

Jeshi la polisi Kenya limewauwa kwa kuwapiga risasi majambazi wawili mmoja wao akiwa ni jambazi wa kike anayesemekana kuwa ni jambazi mrembo pengine kuliko wote.

Majambazi hao waliuwawa wakiwa katika eneo la Chokaa Jijini Nairobi walipopambana na polisi kwa kufyatuliana risasi, huku wenzao wawili wakifanikiwa kutoroka.

Mitandao ya jamii imemtambua jambazi huyo mwanamke kwa jina la Claire Mwaniki, ambaye alikufa mkononi akiwa ameshikilia bastola aina ya Baretta ikiwa na risasi sita.

Kamanda wa Polisi Jijini Nairobi, Japheth Koome, amesema kuwa wahalifu wengi nchini humo wanakuwa na wanawake wanaofanyanao ujambazi.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni