.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 30 Mei 2017

JENERALI MANUEL ANTONIO NORIEGA AFARIKI DUNIA

Kiongozi wa zamani wa kijeshi wa nchi ya Panama, Jenerali Manuel Antonio Noriega, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 83.

Jenerali Noriega hivi karibuni alifanyiwa upasuaji baada ya kuugua tatizo la kupasuka kwa mishipa ya damu, baada ya kufanyiwa upasuaji wa kichwa.

Noriega alikuwa mshirika mkuu wa Marekani na aling'olewa madarakani kwa nguvu wakati vikosi vya Marekani vilipoivamia Panama mwaka 1989 na baadaye kufungwa Marekani kwa makosa ya dawa za kulevya na utakatishaji fedha.

Baadaye aliishia kuwa gerezani, na kisha kuhamishiwa Panama kwa makosa ya mauaji, rushwa na wizi wa fedha.

Baadaye Jenerali Noriega aliachiwa na kuhamishiwa chini ya uangalizi akiwa nyumbani mwezi Januari akijiandaa kwa upasuaji wa uvimbe kichwani mwezi Machi.
Jenerali Manuel Antonio Noriega akisaidiwa kuingia nyumbani kwake baada ya kuhamishiwa chini ya uangalizi akiwa nyumani

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni