.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 12 Mei 2017

MAN UNITED YATINGA FAINALI YA LIGI YA UROPA HUKU PRESHA IKIPANDA NA KUSHUKA

Manchester United imenusurika tishio la dakika za mwisho na kuwatoa wageni Celta Vigo na kufanikiwa kukata tiketi ya kutinga fainali ya Ligi ya Uropa dhidi ya Ajax.

Ikiongoza kwa goli 1-0 katika mchezo wa kwanza, United ilianza kwa kuumiliki mchezo wa jana na kufunga goli la kichwa kupitia kwa Marouane Fellaini kupitia pande la Marcus Rashford.

Lakini Celta, iliyokuwa ikihitaji kufunga magoli mawili, ilisawazisha goli hilo kupitia kwa mchezaji wao Facundo Roncaglia na kuufanya mchezo huo kwa wa roho juu.

Katika mchezo huo mchezaji wa Manchester United Eric Bailly na Roncaglia walitolewa nje kwa kupigana huku wenyeji wakigangamala na kutinga fainali.
                                              Marouane Fellaini akifunga goli kwa mpira wa kichwa
             Mpira uliopigwa na mchezaji Facundo Roncaglia ukiwa umetinga wavuni
                              Fellaini akimzuia Eric Bailly aliyempiga ngumi John Guidetti

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni