.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 31 Mei 2017

MLIPUKO WATIKISA JIJI LA KABUL NA KUUWA WATU WAPATAO 60

Mlipuko mkubwa uliotokea karibu na eneo la majengo ya ubalozi na karibu na makazi ya rais umetikisa Jiji la Kabul nchini Afghanistan.

Maafisa wa Afghanistan wamesema kuwa karibu watu 60 wamepoteza maisha ama kujeruhiwa kwa mlipuko huo hata hivyo wataalam wanaamini idadi inaweza kuongezeka.

Taarifa za awali zinasema mlipuko huo umetokea kwenye gari katika eneo la Zanbaq ambapo nyumba zilizokuwapo umbali wa mita 100 zimeharibika.

Picha za kwenye mitandao ya jamii zinaonyesha moshi mkubwa ukitanda juu ya Jiji la Kabul na magari kadhaa yakiwa yameharibiwa.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni