.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 31 Mei 2017

RIYAD MAHREZ ASEMA ANATAKA KUONDOKA LEICESTER CITY SASA

Mshambuliaji wa Leicester, City Riyad Mahrez, ametangaza kuwa anataka kuondoka katika klabu hiyo.

Mchezaji huyo aliyejiunga na Leicester akitokea klabu ya Ufaransa ya Le Havre kwa kitita cha paundi 400,000 mwaka 2014, amesema alikubali kubakia timu hiyo mwaka jana baada ya kutwaa ubingwa na kuongea na Mwenyekiti wa klabu.

Hata hivyo amesema anamipango mikubwa ya baadaye hivyo basi ameiarifu klabu kuwa anafiriki sasa ni wakati muafaka kwa yeye kuondoka Leicester.

Mahrez, mshindi wa Tuzo ya Wachezaji Bora wa Kulipwa kwa mwaka 2016, ameshuka dimbani mara 48 akiwa na Leicester City katika msimu huu.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni