.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 19 Agosti 2017

TIMU YA MANCHESTER UNITED YAENDELEZA WIMBI LA USHINDI MNONO EPL

Timu ya Manchester United imefunga magoli matatu ndani ya dakika nne na kuendeleza wimbi la ushindi kwa kuibuka na ushindi wa magoli 4-0 dhidi ya Swansea.

Katika mchezo huo Eric Bailly, Romelu Lukaku, Paul Pogba na Anthony Martial walifanikisha kupatikana kwa ushindi huo wa kikosi cha Jose Mourinho.

Jordan Ayew alikuwa wa kwanza kukosa kosa goli kwa kupiga shuti lililogonga mwamba, kabla ya baadaye Eric Bailly kuipatia Manchester United goli la kuongoza.

Romelu Lukaku aliongeza goli la pili kwa Manchester United katika dakika ya 80 kwa shuti la karibu kisha Pogba akafunga la tatu kambla ya Anthony Martial kufunga la nne.
Beki Eric Bailly akiuwahi mpira wa kichwa uliopigwa na Paul Pogba uliogonga mwamba na kuuzamisha kimiyani
                                Paul Pogba akifunga kiufundi goli la tatu la Manchester United
                    Anthony Martial akiachia shuti na kufunga goli la nne la Manchester United 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni