.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 19 Agosti 2017

SAIDIO MANE AIPATIA LIVERPOOL USHINDI WAKE WA KWANZA EPL

Sadio Mane ameipatia Liverpool ushindi wake wa kwanza wa Ligi Kuu ya Uingereza kwa kuifungia goli moja na kuifanya Crystal Palace ikubali kipigo cha pili katika msimu huu.

Kikosi cha Jurgen Klopp kilikuwa kama kinaelekea kutoka sare kufuatia kandanda zuri waliotandaza Crystal Palace lakini Mane aliweza kumpoteza kipa Wayne Hennessey.

Crystal Palace, ilifungwa magoli 3-0 nyumbani katika mchezo wa kwanza dhidi ya Huddersfield ilikosa nafasi ya kufunga kabla ya Mane kutikisa nyavu.
Sadio Mane akifunga goli pekee katika mchezo huo likiwa ni goli lake la pili katika msimu huu
                    Sadio Mane akishangilia goli kwa kumrukia kocha wake Jurgen Klopp

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni