Alisema wanahabari inabidi wazielewe vizuri, kuzichambua na kuwafikishia taarifa za utabiri wa hali ya hewa kiusahihi wananchi jambo ambalo litasaidia wananchi na sekta mbalimbali kujipanga kukabiliana na ama athari zitokanazo na utabiri wa hali ya hewa.
"...Semina kama hizi kwanza zinasaidia wanahabari kuelewa masuala mbalimbali yatokanayo na taarifa zetu za utabiri, kisha wao kuelimisha jamii zaidi kuhusiana na taarifa zetu kupitia vyombo vyao mbalimbali vya habari. Kundi hili likielewa vizuri nao watakuwa mabalozi wazuri kufikisha ujumbe kupitia kalamu zao," alisema Dk Agnes Kijazi.
Aidha pamoja na mafunzo hayo, TMA pia ilipokea mrejesho na ushauri kutoka kwa wanahabari ili kuboresha zaidi namna ya utoaji wa taarifa za utabiri wa hali ya hewa kwa umma.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhbEDg8jTmEL3WbHhOnpVmEx2YLnl7xSIOdTw1_8ihrenaQyYko7HUSwYYzUR6PNJO46v9qKqnylTf19lJ2MZj4OEPI8EAQqyDnL8KMwFDYEyEm8_9P9IAxlrP3UyI2XeJnBKh7BkH1e9Go/s640/A+3.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi6ntmCuqubI55pJV0iCv-zkWuAtAcHvNPRDEYCIdggBMzDaB4_S5H1eRWJZUHbmttWmwu2hShSEQ7Sa-JByNu0c0z0fAs1hE4cA9B-0ebC_r5dbyEdEyAmmcz_C5e3QVXE4hFz7x9IionA/s640/A+4.jpg)
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni