Alisema wanahabari inabidi wazielewe vizuri, kuzichambua na kuwafikishia taarifa za utabiri wa hali ya hewa kiusahihi wananchi jambo ambalo litasaidia wananchi na sekta mbalimbali kujipanga kukabiliana na ama athari zitokanazo na utabiri wa hali ya hewa.
"...Semina kama hizi kwanza zinasaidia wanahabari kuelewa masuala mbalimbali yatokanayo na taarifa zetu za utabiri, kisha wao kuelimisha jamii zaidi kuhusiana na taarifa zetu kupitia vyombo vyao mbalimbali vya habari. Kundi hili likielewa vizuri nao watakuwa mabalozi wazuri kufikisha ujumbe kupitia kalamu zao," alisema Dk Agnes Kijazi.
Aidha pamoja na mafunzo hayo, TMA pia ilipokea mrejesho na ushauri kutoka kwa wanahabari ili kuboresha zaidi namna ya utoaji wa taarifa za utabiri wa hali ya hewa kwa umma.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA), Dk Agnes Kijazi (kulia) akizungumza alipokuwa akifungua semina ya kwa baadhi ya waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari juu ya uandishi wa habari za hali ya hewa. Wengine kutoka kulia ni Bi. Mariam Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Huduma Saidizi wa TMA na Mkurugenzi Huduma za Utabiri TMA, Dk. Hamza Kabelwa.
Mkurugenzi
Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA), Dk Agnes Kijazi (kulia)
akizungumza alipokuwa akifungua semina ya kwa baadhi ya waandishi wa
habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari juu ya uandishi wa habari za
hali ya hewa. Wengine kutoka kulia ni Mkurugenzi Matumizi Matumizi ya
Hali ya Hewa, Dk. Ladslaus Chang'a , Meneja Ofisi Kuu ya Utabiri, Samwel
Mbuya, pamoja na Mkurugenzi Huduma za Utabiri TMA, Dk. Hamza Kabelwa.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni