Shambulizi la Blaise Matuidi katika
dakika ya tatu limetosha kuipatia Ufaransa pointi tatu na kuongoza
kundi A, huku ukiwa umebakia mchezo mmoja wa kuwania kutinga fainali
za kombe la dunia.
Kikosi cha Ufaransa kinachonolewa na
Didier Deschamps, kilipata goli hilo lililofungwa na Matuidi baada
kugongeana vyema baina ya wachezaji Lucas Digne na Antoine Griezmann
na kuizamisha Bulgaria.
Wakati Sweden wakisafiri kwenda
Uholanzi katika mchezo wao wa mwisho wakiwa pointi moja nyuma,
Ufaransa sasa inaweza kukata tiketi ya kutinga fainali za kombe la
dunia jumanne iwapo itaifunga Belarus.
Mfaransa Blaise Matuidi akijipinda na kufunga goli pekee katika mchezo huo
Kiungo wa Chelsea N'Golo Kante akishikilia misuli ya paja wakati akitoka nje baada ya kuumia



Hakuna maoni :
Chapisha Maoni