Cristiano Ronaldo ametokea benchi na
kuisaidia Ureno kuifunga Andorra magoli 2-0 na kuhuisha ndoto yao ya
kutinga fainali za kombe la dunia.
Nyota huyo wa Real Madrid alifunga
goli katika dakika ya 63 kabla baadaye Andre Silva kukamilisha
ushindi kwa kuongeza la pili.
Kwa ushindi huo Ureno ipo nyuma kwa
tofauti ya pointi tatu na vinara wa kundi lao B, timu ya Switzerland,
iliyoifunga Hungary magoli 5-2 huko Basel.
Ureno inahitaji kushinda mchezo wao
wa mwisho katika kundi hilo dhidi ya vinara Switzerland siku ya
jumanne ili iongoze kundi hilo.
Mshambuliaji nyota Cristiano Ronaldo akiifungia Ureno goli katika mchezo huo
Andre Silva akishangilia baada ya kutumbukiza mpira wavuni na kuiandikia Ureno goli la pili



Hakuna maoni :
Chapisha Maoni