Makamu wa Rais wa Chama cha
Wasafirishaji Tanzania (TAT), Omar Kiponza akizungumza na vyombo vya
habari kuelezea kero mbalimbali zinazowakabili wanachama wake leo
katika ofisi za chama hicho jijini Dar es Salaam.
Na. Joachim Mushi
CHAMA cha Wasafirishaji Tanzania
(TAT) imeilalamikia TANROADS kwa kile kukamata magari ya wanachama
wao kwa madai kuwa yameegeshwa eneo ambalo si sahihi, ilhali hakuna
eneo maalumu kwa ajili ya maegesho ya magari makubwa.
Akizungumza leo jijini Dar es Salaam
Makamu wa Rais wa Chama cha Wasafirishaji Tanzania (TAT), Omar
Kiponza alisema baadhi ya barabara ambazo magari ya wanachama wao
wamekuwa wakipita kila siku hakuna sehemu maalum ya maegesho hivyo
utaratibu unaotumiwa kuvuta magari bila ridhaa yanapokamatwa sio wa
kiungwana hivyo kushauri mamlaka husika kukutana na viongozi wa TAT
kupata suluhu la suala hilo.
"...wamekuwa wakivuta magari
bila kutaka maelezo hata kama gari linaweza kutembea lenyewe na kosa
kubwa wanalosema ni kwamba umepaki kwenye road reserve hata kama
dereva amesimama kwa ajili ya dharura ya posho au document
wanakuambia gari iondolewa iende misugusugu na fine wanazotoza huwa
ni kubwa mno. Ikiwa mwanachama wetu atafanya gereji Barabarani au
kufunga njia kwa uzembe basi hapo hatuna pingamizi lolote sheria
ifuate mkondo wake na hatuwezi kutetea uharibifu wa miundombinu ya
nchi yetu," alisema Omar Kiponza.
Alisema kutokana na suala la
mkanganyiko wa uzidishaji mzigo wameiomba TANROADS kuweka mzani
bandarini kama walivyoomba awali ili kuondoa mkanganyiko huu. Alisema
gari linaweza kupima mizani miwili na kuonekana lipo sahihi lakini
likifika mzani wa tatu linaambiwa limezidisha na kutozwa faini jambo
ambalo ni utata mkubwa.
"...Kuna suala la mizani
kutofanyiwa 'calibration' hili suala limekuwa likizunguziwa kwa muda
mrefu sana na mizani mingi haina uwiano katika usomaji, tunawaomba
muliangalie suala hili kwa umakini ili sote tufanye kazi kama
marafiki.
Upande wa mamlaka ya mapato Tanzania
yaani TRA pia kumekuwa na kero ambayo wanachama wetu wanapenda kutoa
malalamiko hii ni juu ya suala la utozaji wa faini ya shilingi elfu
40,000 endapo gari litakuwa halijavuka mpaka ndani ya siku7 pale
tunduma,"
Aidha alisema kero nyingine ni kwa
mamlaka ya SUMATRA ambapo imekuwa ikitoza wanachama wao gari la mzigo
ambalo halifanyi kazi tangia linunuliwe kwa madai ni utaratibu, jambo
ambalo wanaamini ni uonevu.
"Unakuta ulinunua gari la
mizigo bovu au lilisimama kufanya kazi kwa miaka ukienda kuomba
leseni ya usafirishaji unatozwa faini kwa kitu ambacho hakijawahi
kutembea kwa kisingizio kuwa faini hiyo ni kwa ajili ya part
registration sasa faini ya nini kwa kitu ambacho hakijatumika?"
"Vivyo hivyo kuna jambo lingine
linalohusisha watu wa maliasili pindi magari yanapopakiwa mkaa na
madereva siyo kwa ruhusa ya tajiri lakini wanapokamatwa adhabu yote
ya faini analipishwa tajiri wakati huo huo dereva hapewi adhabu
yoyote je hii ni sawa kweli,kwa sababu kuna wasafirishaji ambao
washapigwa faini kama milioni 24 kwa sababu ya mkaa je mamlaka husika
wanafahamu hili au ni sheria watu wanajichukulia mikononi ?" alimalizia kwa kohoji Bw. Kiponza.
Mwisho
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni