.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 11 Oktoba 2017

MIUJIZA YA LIONEL MESSI YAIPELEKA ARGENTINA KOMBE LA DUNIA

Miujiza ya Lionel Messi imeisaidia Argentina kukata tiketi ya fainali za kombe la dunia Urusi 2018, baada ya nyota huyo wa Barcelona kuifungia timu yake ya taifa hat-trick.

Argentina ilifanikiwa kujihakikishia nafasi hiyo baada ya kuibuka na ushindi wa magoli 3-1 dhidi ya Ecuador huko Quito jana.

Romario Ibarra aliipatia Ecuador goli la kuongoza kabla ya Lionel Messi kusawazisha kufuatia kugongena vyema na Angel Di Maria.

Messi tena akafunga goli la pili kwa shuti la mguu wake wa kushoto na kisha akakamilisha hat-trick yake ya 44 katika maisha yake ya soka baada ya dakika ya 62.
                   Lionel Messi akishangilia kwa kubeba mpira baada ya kufunga goli la kwanza
                    Lionel Messi akitumbukiza goli la pili huku akiwaacha hoi mabeki wa Ecuador

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni