Maelfu ya walimu wa shule za msingi
Nigeria katika jimbo la Kaskazini la Kaduna watafukuzwa kazi baada ya
kushindwa kufaulu mtihani uliotungwa kwa ajili ya wanafunzi wa miaka
sita.
Gavana wa jimbo hilo Nasir El-Rufai
amesema kati ya walimu 21,780, theluthi mbili wameshindwa kufikisha
alama 75 ambayo ndio kiwango cha ufaulu kilichopangwa kwa wanafunzi
wao.
Gavana El-Rufai amesema wataajiri
walimu wapya 25,000 ili kuziba nafasi za walimu ambao wameshindwa
kufaulu mtihani wa wanafunzi wao ambao watatimuliwa kazi.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni