.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 11 Oktoba 2017

NYOTA KADHAA KUTOONEKANA KATIKA FAINALI ZA KOMBE LA DUNIA

Wakati timu zilizofuzu kutinga fainali za kombe la dunia zikijulikana, michuano hiyo itawakosa nyota kadhaa ambao timu zao za taifa hazijafanikiwa kupata tiketi ya michuano hiyo.

Miongoni mwa wachezaji hao ni Arjen Robben, wa Uholanzi na timu ya Bayern Munich, kiungo Christian Pulisic, wa Marekani na klabu ya Borussia Dortmund.

Wengine ni kiungo Arturo Vidal wa Chile na timu ya Bayern Munich, kiungo Naby Keita, wa Guinea na klabu ya RB Leipzig pamoja na Gareth Bale wa Wales timu ya Real Madrid.

Pia wamo Pierre-Emerick Aubameyang wa Gabon na klabu ya Borussia Dortmund, Alexis Sanchez wa Chile na timu ya Arsenal, Antonio Valencia wa Ecuador na Manchester United.
                               Mshambuliaji Gareth Bale hatashiriki fainali za kombe la dunia
                  Arturo Vidal wa Chile naye hataonekana Urusi kwenye kombe la dunia
                     Pierre-Emerick Aubameyang wa Gabon naye hatokuwepo Urusi 2018

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni