Patrice Evra ametolewa nje ya uwanja
baada ya kumpiga teke la kichwani mmoja shabiki wa timu yake kabla ya
mchezo wa ligi ya Uropa ambao Marseille ilifungwa na Vitoria
Guimaraes.
Picha zinamuonyesha beki huyo wa
zamani wa Manchester United akimrukia teke shabiki wao uwanjani
wakati timu zikipasha kabla ya mechi.
Bodi ya nidhamu ya UEFA inatarajiwa
kutoa hatua zaidi za adhabu dhidi ya Patrice Evra hii leo.
Patrice Evra akiondolewa na wachezaji wenzake asiendeleze ubabe wake
Akiwa Manchester United Patrice Evra aliwahi kupigana na mmoja wa wasimamizi wa uwanja wa Chelsea
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni