Timu ya Arsenal imetinga hatua ya
mtoano ya Ligi ya Uropa licha ya kutoka sare tasa na Red Star
Belgrade.
Mshambuliaji Olivier Giroud,
anapaswa kujilaumu kwa kukosa nafasi kadhaa za kufunga na mara mbili
mashambulizi yake yalizuiliwa na kipa Milan Borjan.
Nafasi bora kabisa ya kufunga katika
mchezo huo ilimkuta kiungo Jack Wilshere, lakini shuti lake
liliokolewa kwenye mstari wa goli.
Kipa wa Arsenal Matthew Macey akipangua mkwaju wa Vujadin Savic
Kiungo wa Arsenal Jack Wilshere akijaribu kufunga goli katika mchezo huo
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni