Everton waliobakia 10 uwanjani
wametolewa nje ya Ligi ya Uropa baada ya kuchapa magoli 3-0 na Lyon,
na kutibua matumaini ya David Unsworth kuteuliwa kuwa kocha wa kudumu
wa timu hiyo.
Mchezaji wa zamani wa Chelsea
Bertrand Traore alianza kutikisa nyavu katika dakika ya 68 baada ya
kuwazidi kasi mabeki wa Everton na kutumbukiza mpira uliomshinda kipa
Jordan Pickford.
Mambo yalizidi kuwa magumu pale
Morgan Schneiderlin alipopewa kadi ya pili ya njano kwa kumchezea
rafu Maxwel Cornet.
Mchezaji wa zamani wa Manchester
United Memphis Depay alimpa pande Houssem Aouar na kufunga la pilina
kisha baadaye Depay akakamilisha karamu kwa kufunga goli la tatu.
Morgan Schneiderlin akitoka nje baada ya kuonyeshwa kadi nyekundu
Mchezaji wa zamani wa Chelsea
Bertrand Traore akifunga goli
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni