Mshambuliaji Sergio Aguero amekuwa
mfungaji aliyeifungia Manchester City magoli mengi katika kipindi
chote wakati wakiifunga Napoli kwa magoli 4-2 na kutinga hatua ya
mtoano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Katika mchezo huo Manchester City
ilitokea nyuma na kuibuka na ushindi na kuifunga Napoli ambayo
haijafungwa hadi sasa katika ligi ya Serie A. Lorenzo Insigne
aliifungia Napoli goli la kwanza.
Nicolas Otamendi akafunga goli la
kusawazisha Jone Stones kaongeza goli la pili, Frello Fillo
akaifungia Napoli goli la pili, kisha Sergio Aguero akaifungia
Manchester City goli la tatu na baadaye Raheem Starling.
Kipa wa Napoli akiruka bila ya mafanikio mpira uliopigwa na Jone Stones
Mshambuliaji Sergio Aguero akiachia shuti na kufunga goli la tatu la Man City
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni