.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 28 Januari 2018

WAKAZI WA MJI WA CAPE TOWN WATAKIWA KUBANA MATUMIZI YA MAJI

Wakazi wa Mji wa Cape Town nchini Afrika Kusini wametakiwa kuhifadhi maji kama vile maisha yao yanategemea maji, ili kuepusha kufungwa kwa huduma ya maji.

Ukame mkali umelazimisha Manispaa ya Jiji hilo kudhibiti matumizi kufikia lita 50 sawa na galoni 11 kwa mtu mmoja kwa siku.

Maafisa wa Jiji la Cape Town wamewasihi watu kuacha kutumia maji ya kuflash chooni, ili kuhifadhi maji.

Mkuu wa serikali ya Mkoa wa Cape Town amesema kuwa iwapo mabomba yatakosa maji itakuwa ni janga juu ya janga.
   Wakazi wa Jiji la Cape Town wakiwa kwenye foleni ya maji baada ya maji kuadimika
   Wakazi wa Jiji la Cape Town wakiwa na madumu wakihaha kutafuta maji yaliyoadimika

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni