.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 4 Aprili 2018

RONALDO AFUNGA GOLI TAMU LA TIKI TAKA HUKU AKIWEKA REKODI

Cristiano Ronaldo amefunga moja ya magoli mazuri katika Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa staili ya tik taka na kuisaidia Real Madrid kuichakaza Juventus kwa magoli 3-0 katika mchezo wa kwanza wa robo fainali.

Katika mchezo huo ambao Ronaldo alifunga magoli mawili lakini lilikuwa goli la tiki taka ambalo halitosahaulika na liliwakuna hata wapinzani wao Juventus ambapo mashabiki wa timu hiyo walimpongeza.

Ronaldo pia aliweka rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza kufunga magoli 10 mfululizo katika michezo ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, katika mchezo huo ambao ulishuhudia Paulo Dybala akipewa kadi nyekundu katika dakika ya 66.
   Cristiano Ronaldo akifunga goli la kihistoria kwa staili ya tiki taka na kuwashangaza wengi
   Mshambuliaji wa Juventus Paula Dybala akishika kiuno baada ya kuonyeshwa kadi nyekundu.
   Beki Marcelo akifunga goli la tatu la Real Madrid katika dakika ya 74 na kukamilisha ushindi

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni