.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 3 Aprili 2018

WINNIE MADIKIZELA-MANDELA KUZIKWA APRILI 14

Utawala wa kifalme wa Abathembu umesema unaandaa taratibu za maziko ya mwanaharakati wa kupinga ubaguzi enzi za utawala makaburu nchini Afrika Kusini Winnie Madikizela-Mandela katika eneo la Qunu huko Eastern Cape.

Wakati utawala huo ukitangaza maandalizi hayo Rais wa Afrika Kusini Bw. Cyril Ramaphosa amesema kuwa marehemu, Winnie ambaye anatambulika kwa wengi kama Mama wa Taifa atafanyiwa maziko ya kitaifa tarehe 14 mwezi huu.

Kufanyika kwa maziko ya Mama Winnie Mandela Qunu kunatokana na yeye kuolewa mtu wa kutoka ukoo ya kabila la Abathembu ambaye ni rais wa kwanza mwafrika nchini Afrika Kusini hayati Nelson Mandela kwa miaka 38.

Msemaji wa ufalme wa Abathembu, Prince Siganeko Dalindyebo amesema kuwa familia ya kifalme inaona inaowajibu na kutaka mwili wa Winnie uletwe nyumbani Qunu ambapo atapumzika kwa amani, kwani kwa mujibu wa mila hakuwa amepewa talaka.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni