![]() |
| Ronaldo akipeana mkono kwa shingo upande na Mourinho |
Katika mechi hiyo Ronaldo alitikisa
nyavu mara mbili na kutengeneza bao la kwanza dhidi ya timu
inayofundishwa na kocha wao wa zamani Mourinho, ambae aliondoka
Bernabeu mwishoni mwa msimu uliopita na kujiunga na Chelsea.
Baada ya kutandikwa bao la kwanza
Chelsea ilipata bao la haraka haraka la kusawazisha kupitia Ramires,
hata hivyo baada ya hapo ilishindwa kabisa kufurukuta mbele ya Real
Madrid na kujikuta ikiondoka na kipigo cha mabao 3-1.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni