.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 14 Agosti 2013

TABASAMU KIDOGO JUAMATANO YA LEO!!


Traffic mmoja aliyekuwa tayari kapiga kinywaji na kalewa mchana kweupe, jana alilisimamisha gari moja dogo lililokuwa linaendeshwa na mwanamama mmoja wa makamo hivi.

Yule mama baada ya kusimamishwa, akaliegesha gari pembeni akimsubiria yule traffic afike amwambie makosa yake. Alipochungulia kupitia kioo cha pembeni, akamuona yule Traffic akimfuata huku akiyumba kutokana na kuzidiwa na kilevi.

Alipofika huku ananuka pombe, yule Traffic akamwambia yule mama amuonyeshe leseni ya udereva. Yule mama akafungua pochi yake, akatoa kioo kidogo cha kujiangalia wakati anajiremba na kumpa yule Traffic.

Alipokipokea, askari yule wa usalama barabarani akakiangalia kile kioo kwa dakika tano huku kakitolea macho kweli kweli kisha akamrudishia yule mama huku anamwambia:-

" Sasa si ungeniambia na wewe ni traffic mwenzangu, haya nenda ila punguza kuchomekea watakugonga afande"

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni