.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 13 Oktoba 2013

RAIS KIKWETE APOKELEWA KWA NDEREMO MKOANI IRINGA

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwasili Uwanja wa Ndege wa Nduli mjini Iringa leo Oktoba 13, 2013 kuhudhuria Maadhimisho ya Kilele cha Mbio za Mwenye wa Uhuru, Wiki ya Vijana na Kumbukumbu ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere zitaziofabyika kesho (Oktoba 14, 2013) katika uwanja wa Kumbukumbu ya Samora. PICHA NA IKULU.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na kamanda wa vijana Iringa Mhe Asas katika Uwanja wa Ndege wa Nduli mjini Iringa leo Oktoba 13, 2013 kuhudhuria Maadhimisho ya Kilele cha Mbio za Mwenye wa Uhuru, Wiki ya Vijana na Kumbukumbu ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere zitaziofabyika kesho (Oktoba 14, 2013) katika uwanja wa Kumbukumbu ya Samora

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mbunge wa Iringa mjini Mhe Msigwa katika Uwanja wa Ndege wa Nduli mjini Iringa leo Oktoba 13, 2013 kuhudhuria Maadhimisho ya Kilele cha Mbio za Mwenye wa Uhuru, Wiki ya Vijana na Kumbukumbu ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere zitaziofabyika kesho (Oktoba 14, 2013) katika uwanja wa Kumbukumbu ya Samora.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amewasili mjini Iringa jioni ya leo, Jumapili, Oktoba 13, 2013, kwa ziara ya siku mbili ya kikazi mkoani Iringa. Rais Kikwete amefuatana na Mama Salma Kikwete.

Shughuli kubwa ambazo Mheshimiwa Rais atazifanya wakati wa ziara hiyo ni kushiriki Kumbukumbu ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, kuwa mgeni rasmi katika Kilele cha Mbio za Mwenge Kitaifa mwaka huu wa 2013 na Kilele cha Wiki ya Vijana.

Ndege iliyombeba Rais Kikwete ilitua kwenye Uwanja wa Ndege wa Nduli mjini Iringa kiasi cha saa 12.20 jioni na kulakiwa na umati mkubwa wa wananchi wakiwemo wafuasi wa vyama vya siasa vikiwamo CCM na Chadema.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni