.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 13 Desemba 2013

ALIYEPOTOSHA LUGHA YA ISHARA KUCHUNGUZWA NA SERIKALI YA AFRIKA KUSINI

Naibu Waziri wa Wizara ya Walemavu nchini Afrika Kusini amesema serikali ya nchi hiyo inachunguza ni namna gani mtu aliyekuwa akitafsiri kwa ishara wakati wa Ibada ya Kitaifa ya Kumbukumbu ya Mandela alivyoruhusiwa na maafisa usalama kuingia kufanyakazi hiyo.

Mtu huyo Thamsanqa Jantjie, ambaye alisimama pembeni ya viongozi wa dunia katika Ibada hiyo amekanusha kuwa ni tapeli na kusema alichanganyikiwa alipoona malaika wakija katika uwanja na kuanza kupatwa na mawenge.

Taasisi ya Wakalimani wa Lugha za Ishara zinazotumika kwa watu wenye tatizo la kusikia imesema imeshapeleka mara nyingi malalamiko kuhusiana na utendaji kazi mbovu wa Jantjie kwa chama cha ANC, hakijachukua hatua yoyote.

Baada ya kuibuka malalamiko kwa watu wanaotambua lugha ya ishara kuwa mtu huyo alichokuwa anakifanya ni upuuzi na hakikuwa na maana yeyote, ofisi ya wakala iliomuajiri kufanya kazi hiyo nayo imetoweka.



Hakuna maoni :

Chapisha Maoni