Timu ya Chelsea imefanikiwa kuongoza
kundi E na kutinga hatua ya mtoano ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya
kupitia bao pekee lililofungwa na Demba Ba dhidi ya Steaua Bucharest
na kufanya matokeo kuwa 1-0.
Mshambuliaji huyo raia wa Senegal
aliunganisha wavuni wa mpira wa katika mchezo huo ambao wenyeji
Chelsea walitawala dakika zote kumi za mwanza za mchezo huo katika
dimba la Stamford Bridge.
BARCELONA YAUA....
Celtic imepata kipigo cha karne katika
Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya baada ya kuchakazwa na Barcelona kwa mbao
6-1 huku mbrazil Neymar akipachika wavuni mabao matatu yaa hat-trick.
Matokeo mengine ya ligi hiyo ni
Galatasaray 1 - 0 Juventus, FC Schalke 04 2 - 0 Basel, Marseille 1 -
2 Borussia Dortmund, Napoli 2 - 0 Arsenal, Atlético Madrid 2 - 0 FC
Porto,FK Austria Vienna 4 - 1 Zenit St Petersburg na Milan 0 - 0
Ajax.








Hakuna maoni :
Chapisha Maoni