Sunderland imeweza kutinga nusu fainali
ya kombe la Capital One baada ya kuifunga Chelsea bao la pili katika
dakika za ziada na kufanya matokeo ya mchezo huo kuwa 2-1.
Chelsea ilipata bao dakika ya 46 ambalo
mchezaji Cattermole alijifunga, na ndipo Sunderland walipozinduka
dakika ya 88 na kuzawazisha kupitia kwa Borini, na baadae katika muda
wa ziada Ki alipachika bao dakika ya 118.
MAN CITY YASHINDA..........
Edin Dzeko amefumania nyavu mara mbili
wakati Manchester City ikifanikiwa kuingia nusu fainali za kombe la
Capital One katika mchezo walioibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya
Leicester.
Aguero akisindikizwa kutolewa nje ya uwanja baada ya kuumia





Hakuna maoni :
Chapisha Maoni