.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 17 Desemba 2013

WAGONJWA KENYA WATIMULIWA HOSPITALI, KUFUATIA MGOMO UNAOENDELEA

Wagonjwa hapo jana wametimuliwa kwenye hospitali za umma mashariki mwa Kenya, kufuatia mgomo wa watumishi wa afya unaoendelea.

Ndugu za wagonjwa walikusanyika kwenye vituo vya afya kuchukua wagonjwa wao wakati mgomo wa watumishi wa umma ukiingia siku ya saba.

Katika hospitali ya rufaa ya Jaramogi Oginga Odinga iliyopo Kisumu kunataarifa kuwa wagonjwa waliondolewa kwa nguvu kutoka vitandani na walinzi wa hospitali hiyo.

Hospitali ya wilaya ya Kisumu imefungwa lakini wagonjwa ambao hawana ndugu kuwasaidia kuweza kutoka wamebakia katika hospitali hiyo iliyotelekezwa.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni