.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 18 Desemba 2013

WAJAWAZITO WAPOTEZA WATOTO WANANE KUFUATIA MGOMO WA MADAKTARI


Hospitali ya Taifa ya Kenyatta nchini Kenya imesema watoto wachanga wanane wamekufa kabla ya mama zao kujifungua kutokana na ukosefu wa huduma za afya kutoka na mgomo wa madaktari unaoendelea.

Aidha kitengo cha watoto njiti pamoja na wale wenye matatizo mbalimbali katika hospitali hiyo kimezidiwa na watoto kutokana na watoto kutolewa kwenye hospitali hiyo kutokana na kukosekana kwa huduma kwenye hospitali zingine za umma.

Kutokana na hali hiyo kitengo hicho chenye uwezo wa kulaza watoto 40 katika vizimba vya kukuzia watoto njiti, kina watoto 122 hali inayofanya watoto watatu hadi watano kuchangia kizimba kimoja, kinachopaswa kulaza mtoto mmoja.


Hakuna maoni :

Chapisha Maoni