Mamia ya watu inaaminika wamekufa
kwenye mapambano nchini Sudan Kusini yanayohusisha majeshi ya
serikali na kundi lililojitenga.
Wanadiplomasia wa Umoja wa Mataifa
wameambiwa na vyanzo mbalimbali vya habari katika Mji Mkuu wa Juba
kuwa vifo vinaweza kuwa kati ya watu 400 hadi 500.
Sudan Kusini imekuwa kwenye siku mbili
za machafuko, kufuatia taarifa ya kutokea jaribio la mapinduzi dhidi
ya Rais Salva Kiir.
Taarifa za awali zilisema maafisa 10 wa
ngazi za juu serikalini, akiwemo Waziri wa Fedha wamekamatwa kwa
kuhusishwa na jaribio hilo la kupindua serikali.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni