.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 28 Januari 2014

MAAFISA KILIMO ZAIDI YA 40 WA WILAYA YA KALAMBO WAKUTANA KUWEKA MKAKATI WA KUINUA UZALISHAJI KWA WAKULIMA


Mkuu wa wilaya ya Kalambo Moshi Chang'a akizungumza na maafisa ugani wa Halmashauri ya wilaya ya Kalambo alipofungua kikao kazi chao cha siku mbili jana katika kijiji cha Msanzi kata ya Msanzi wilayani humo 
Mkuu wa wilaya ya Kalambo Moshi Chang’a akizungumza na maafisa ugani wa Halmashauri ya wilaya ya Kalambo alipofungua kikao kazi chao cha siku mbili jana katika kijiji cha Msanzi kata ya Msanzi wilayani humo

NA RAMADHANI JUMA,KALAMBO

Zaidi ya Maafisa kilimo 40 wa wilaya ya Kalambo wanakutana kwa muda wa siku mbili katika kikao kazi kwa lengo la kujadili na kuweka mikakati ya kuinua uzalishaji na kuwainua wakulima wa wilaya hiyo ili waondokane na hali ya umasikini.

Kikao kazi hicho kinachofanyika katika kijiji cha Msanzi wilayani humo ni sehemu ya utekelezaji wa Mpango wa serikali wa “Matokeo Makubwa Sasa” katika sekta ya kilimo.
 
Akifungua kikao kazi hicho, Mkuu wa wilaya ya Kalambo Moshi Chang’a aliwataka Maafisa hao kuwa mfano wa kuigwa na wakulima wa wilaya hiyo kwa  kuwa na mashamba yao yaliyolimwa kisasa.
 
Aliwataka pia kuhakikisha kila kata na vijiji wanakofanyia kazi kunakuwa na shamba darasa lenye ukubwa  usiopungua robo eka kwa ajili kutolea mafunzo kwa wakulima, sambamba na utunzaji wa takwimu halisi kwa vpindi tofauti ili kuwa utendaji kazi wenye tija na unaopimika.

Aliwaagiza pia kusimamia kwa karibu utekelezaji wa kila shule ya msingi na sekondari wilayni kulima shamba lisilopungua ekari tano ili wanafunzi wapate uhakika wa chakula wakati wa masomo kwa lengo la kuinua kiwango cha ufaulu.

Mwishoni mwa mwaka jana, mkuu huyo wa wilaya alitangaza mpango wa kuzipatia shule zote wilayani humo vocha tano za pembejeo ili zifanikishe uzalishaji wa chakula cha wanafunzi wanapokuwa masomoni 

Wilaya ya Kalambo yenye Kata 17 na Vijiji 100 ina maafisa kilimo zaidi ya 40 waliopo katika kata na vijiji hivyo.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni