.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 29 Januari 2014

SHIRIKA LA UNESCO LAONYA JUU YA ATHARI YA KIWANGO DUNI CHA ELIMU

Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni UNESCO limeonya kwamba kiwango duni cha Elimu kinachotolewa kinajenga ongezeko kubwa la watu wasiojua kusoma kuliko inavyodhaniwa.

Ripoti mpya iliyotolewa na shirikisho hilo la UNESCO inaonyesha kuwa takribani watu milioni 175 katika nchi masikini, robo ya idadi hiyo ikiwa ni
vijana hawawezi kuandika au kusoma sentensi moja iliyokamilika.

Ripoti hiyo inaonyesha kuwa katika nchi nyingi za Kusini mwa Sahara idadi ya watoto kati ya wainne hadi watano kutoka katika familia masikini
wanamaliza elimu ya msingi bila kujifunza kanuni za awali za kusoma na kuhesabu.

Shirika la UNESCO limesema dola bilioni 130 hupotezwa kwa kutumika visivyo kila mwaka kutokana na elimu duni.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni