.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 29 Januari 2014

CHAMA TAWALA CHA ZANU-PF CHATAFUTA FEDHA ZA BIRTHDAY YA MUGABE

Chama Tawala nchini Zimbabwe Zanu-PF kinapanga kuchangisha dola milioni moja kwa ajili ya sherehe ya kuadhimisha siku ya kuzaliwa rais Robert Mugabe ambaye atatimiza umri wa miaka 90 mwezi ujao.

Katibu wa Masuala ya Vijana wa chama cha Zanu-PF Absalom Sikhosana amekaririwa na mtandao wa newzimbabwe.com kuwa maandalizi kwa ajili ya shuhguli hiyo maalumu yanaendelea vizuri.

Rais Mugabe ataadhimisha siku ya kuzaliwa Februari 21 lakini sherehe zimepangwa kufanyika Februari 23 huko Marondera.

Kiongozi huyo aliyezaliwa mwaka 1924, ameitawala nchi hiyo tangu mwaka 1980 na ni kiongozi mzee zaidi kuliko wote barani Afrika.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni