.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 29 Januari 2014

MWEZI MMOJA MICHAEL SCHUMACHER HOSPITAL

Mwezi mmoja baada ya kujeruhiwa katika ajali ya mchezo wa kuteleza kwenye barafu, meneja wa bingwa wa mashindano ya mbio za magari ya langalanga, Mjerumani Michael Schumacher amesema kwamba madaktari wanaendelea kumwangalia kwa karibu kwani hali yake kiafya bado haijatengemaa.
Bingwa huyo mara saba aligonga kichwa chake katika mwamba wakati akiteleza kwenye barafu katika milima ya Alps nchini Ufaransa.
Madaktari wanatumia madawa kumpa usingizi wakijaribu kupunguza uvimbe na kuchubuka kwenye ubongo wake.
Tayari wamemfanyia upasuaji mara mbili kuondoa damu iliyoganda kwenye ubongo.
Hata hivyo huenda maisha yake yakawa hatarini iwamo ataendelea kuwa katika hali ya kuzirai kutokana na hatari ya ubongo wake kuharibika na kupata maambukizi ya kifua.
Mashabiki wa Michael Schumacher wakati wa maadhimisho ya siku yake ya kuzaliwa nje ya hosipitali alikolazwa

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni