.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 26 Februari 2014

MAHAKAMA NCHINI MISRI IMEWAHUKUMU ADHABU YA KIFO WATU 26


Mahakama nchini Misri imewahukumu adhabu ya kifo watu 26 kwa kosa la kuanzisha kikundi cha kigaidi kwa lengo la kushambulia meli zinazopita katika mfereji wa Suez.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Misri watu hao pia wametuhumiwa kutengeneza mabomu na milipuko mingine mbalimbali, ambapo hukumu hiyo imetolewa leo bila wao kuwepo mahakamani.

Hukumu hiyo imekuja siku moja tu baada ya Waziri Mkuu mpya mteule Ibrahim Mahlab kuapa kuuvunja ugaidi katika kona zote za nchi hiyo.

Bw. Mahlab ameteuliwa kuunda serikali mpya ya nchi hiyo baada kujiuzulu ghafla kwa Waziri Mkuu wa mpito Hazem Beblawi na baraza lake lote siku ya Jumatatu.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni