Hatimaye
bendi kongwe, bendi pekee ambayo imepata kuwa mabingwa wa muziki nchini mara zote
mbili ambazo mashindano hayo yamepata kufanyika, bendi ya Mlimani Park Orchestra “Sikinde Ngoma ya Ukae”
imeanza kuipua nyimbo zake mpya zitakazokuwa katika album mpya ya “Jinamizi la
Talaka” itakayozinduliwa mwaka huu 2014.
Album
hiyo itakuwa na jumla ya nyimbo 7. Mpaka
sasa Sikinde wameishazitoa nyimbo tatu za 1. Jinamizi la
Talaka, 2. Za Mkwezi Mbili na 3. Nikipata
Nitalipa.
Nyimbo
hizi unaweza kuzisikiliza online au ku-download kwenye mtandao wa https://www.hulkshare.com/ sikinde
Nyimbo
4 zilizobakia ambazo nazo zitatolewa muda wowote kuanzia hivi sasa ni 1. Kibogoyo, 2. Dole Gumba, 3. Ng'ombe Haelemewi na Nundu na 4. Tabasamu
Hii ni album ya kwanza kutolewa tokea mwaka 2009 iliporekodiwa album ya “Supu Umeitia Nazi” album iliyomfanya mwimbaji wake Karama Regesu kuchukua zawadi katika Kili Music Award ya mwaka 2009 kwenye category ya “Mtunzi Bora wa Muziki
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni