Benki ya dunia imesitisha msaada wa dola milioni 90 kwa
Uganda ,ikiwa ni siku chache tu baada ya Rais Yoweri Museveni wa nchi hiyo kupitisha
sheria mpya ya kupiga marufuku mapenzi ya jinsia moja.
Benki hiyo imesema kuwa inataka kufanya tathmini yake kuhakikisha kuwa malengo yake ya maendeleo nchini Uganda katika sekta ya afya, ambayo msaada huo ulikuwa umeelekzwa, hayataathirika .
Sheria iliyoidhinishwa na Rais Yoweri Museveni, ilitiwa saini Jumatatu na inatoa adhabu kali kwa watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja.
Wafadhili wengine tayari wameanza kusitisha misaada Uganda. Wahisani kama Denmark na Norway wamesema kuwa wataanza kufadhili mashirika moja kwa moja badala ya serikali.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni