Chama cha Wanasheria nchini Kenya (LSK)
leo kimetishia kutaka kuondolewa kwa mkuu wa jeshi la polisi nchini
humo IGP David Kimaiyo ikiwa atashindwa kutii amri ya mahakama ya
kumkamata Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani, Mutea Iringo.
Mwenyekiti wa LSK Eric Mutua amesema
kitendo cha kutokutii amri ya mahakama kilichofanywa na Kimaiyo ni
msingi wa kuondolewa madarakani, hatua ambayo LSK itachukua iwapo
atashindwa kutekeleza amri halali ya mahakama.
Jaji George Odunga aliamuru Katibu Mkuu
Iringo kukamatwa baada ya kushindwa kulipa fidia ya shilingi milioni
31 kwa raia wa Tanzania aliyewekwa kizuizini kimakosa na kuteswa.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni