Kesi ya mwanariadha wa Afrika Kusini
Oscar Pistorius ya kumuua rafiki wake wa kike mwanamitindo Reeva
Steenkamp imeanza nchini Afrika katika mji wa Pretoria.
Pistorius alimpiga risasi Steenkam
ambaye ni modo na muigizaji wa kwenye runinga, nyumbani kwake
Pretoria Februari 14 mwaka 2013.
Waendesha mashtaka wa serikali wanadai
mauaji hayo yalipangwa, lakini mwanariadha huyo anayetumia miguu ya
bandia amedai alidhani kuwa amevamiwa na mtu na ndipo alipomfatulia
risasi mpenzi wake.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni