Wapiganaji wanaohisiwa kuwa ni wa kundi
la Boko Haram wamewauwa kwa kuwapiga risasi watu 39 katika kijiji
kimoja Kaskazini Mashariki mwa Nigeria.
Washmbuliaji hao wamekiteketeza kijiji
hicho cha Mainok kilichopo kilomita 50 Magharibi mwa Mji wa
Maiduguri.
Tukio hilo limetokea jumamosi, ikiwa ni
baada ya saa mbili kupita tangu kutokea kwa milipuko miwili iliyoua
watu wapatao 50 huko Maiduguri.
Kundi la Boko Haram limekuwa
likiendesha kampeni za miaka 4, kudai sheria za Kiislam Kaskazini mwa
Nigeria.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni