Wachezaji Luis Suarez, Sterling na nahodha Steven Gerald jana walifunga bao moja moja na kuisaidia timu yao ya Liverpool kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Southampton katika mchezo wa ligi kuu ya Uingereza.
Suarez alifunga dakika ya 16, Sterling aakaongeza la pili dakika ya 58 kabala ya Gerald kuhitimisha karamu ya mabao kwa kufunga kwa penati kunako dakika ya 90.
Sterling akifunga bao la pili huku mlinda mlango wa Southampton akiwa hana la kufanya


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni