Shirika la Mslaba Mwekundu limesema
milipuko miwili iliyolenga basi kwenye soko la mji wa Maiduguri
Kaskazini Mashariki mwa Nigeria imeua watu wapatao 50.
Vyanzo kutoka kwenye hospitali vimesema
wengi wa waliodhurika na tukio hilo ni watoto.
Mji wa Maiduguri ni makao makuu ya
vikosi vya jeshi vinavyopigana na kundi la Kiislam la Boko Haram,
ambalo limezidisha mashambulizi yake kwa raia hivi karibuni.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni