Oscar Pistorius ameangua kilio leo
mahakamani wakati wakili wake alipokuwa anajenga hoja kuwa mpenzi
wake Reeva Steenkamp alikuwa amedhurika mno ubongo kutokana na risasi
alizopigwa, kiasi cha kushindwa kuweza kupiga mayowe kama
ilivyodaiwa.
Wakili Barry Roux ametoa madai hayo
katika kujibu ushahidi wa jirani wa Pistorius ambaye alidai
mahakamani kuwa alisikia marehemu Reeva akipiga mayowe na kisha
kusikia risasi katika usiku ambao modo huyo aliuwawa.
Wakili huyo ameiambia mahakama
kutatolewa ripoti kuwa madaktari kuonyesha ubongo wa marehemu
ulivyoharibika kutokana na risasi, hali ambayo haiwezekani kupiga
mayowe. Kauli hiyo ilimfanya mtuhumiwa wa mauaji hayo Oscars kuziba
masikio yake kwa mikono na kuangua kilio.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni