Shahidi wa upande wa Jamhuri Charl
Johnson katika kesi inayomkabili mwanariadha mlemavu wa Afrika Kusini
Oscar Pistoria amesema amepata usumbufu kutokana na namna yake ya
simu kusomwa hadharani kwenye Mahakama Kuu ya Gauteng Kaskazini.
Amesema kuwa tangu siku hiyo simu yake
imekuwa ikiita mno na kupokea ujumbe wa vitisho na kumtuhumu kuwa
kwanini amedanganya kuhusiana na tukio la usiku aliouwawa Reeva
Steenkamp na mpenzi wake Osacr Pistoria.
Namba ya simu ya Johnson ilisomwa
mahakamani siku ya Jumanne, jambo ambalo hakuwa analifahamu hadi
alipoanza kupokea simu hizo na ujumbe wa vitisho.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni