Waziri mkuu wa China, Li Keqiang, ameuambia mkutano wa kila mwaka wa bunge la taifa hilo mjini Beijing, kwamba maendeleo ya kiuchumi yanasalia kuwa jukumu kubwa zaidi la serikali, lakini marekebisho ya kimsingi ni sharti yatekelezwe japo ni machungu.
Bwana Li amewaambia maelfu ya wajumbe katika bunge la taifa hilo, Great Hall of the People, kwamba shabaha ya kila mwaka ya ukuaji wa kiuchumi itasalia kuwa asilimia saba nukta tano.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni