.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 17 Aprili 2014

KUZAMA KWA KIVUKO KOREA KUSINI, WAZIRI MKUU CHUNG-HON APIGWA NA CHUPA YA MAJI

 Waziri Mkuu wa Korea Kusini Chung-Hon won ( mwenye miwani ) akiwa amezungukwa na walinzi wake baada ya kupigwa na chupa ya maji na ndugu wenye hasira kufuatia kuzama kwa kivuko kilichokuwa na abirai 470 na mpaka sasa jumla ya watu 300 bado hawajaonekana. 

Waziri mkuu huyo alikuwa amefika kuwapa pole ndugu waliokuwa wakisubiria kupata taarifa za maendeleo ya zoezi la uokoaji linavyoendelea
 Mmoja wa ndugu waliozama katika kivuko huko Korea Kusini ( kulia ) akimzaba kibao mmoja wa maofisa wa serikali 
 Juhudi za uokoaji ziliendelea hadi usiku kufuatia kuzama kwa kivuko hicho kilichokuwa kinaelekea katika kisiwa cha Kusini cha Jeju. Hadi jana jumla ya watu wanne walikuwa wamefariki dunia, na watu wengine 167 walikuwa wameokolewa huku 300 wakiwa bado hawajaoonekana
 Ndugu wa waliozama na kivuko hicho wakiwa katika juhudi za kuwatafuta ndugu na jamaa zao, japo hali mbaya ya hewa ilikuwa ni kikwazo kikubwa
                                                             Waokoaji wakiwa katika zoezi la uokoaji
Mmoja wa ndugu waliozama na katika kivuko hicho akilia kwa uchungu baada ya ndugu yake kutokuwa mmoja wa waliookolewa mpaka sasa

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni