Ndege ya shirika la ndege ya Marekani jana jioni ilichelewa kuruka kwa muda kutoka uwanja wa ndege wa kimataifa wa JFK kuelekea Washington baada ya mmoja wa husika na usalama wa ndege hiyo kuona ujumbe kupitia akaunti ya Twitter ya shirika hilo, kuwa kuna bomu ndani ya ndege hiyo
Ndege hiyo namba 5714 ilikuwa imepangwa iruke kutoka uwanja wa kimataifa wa John F. Kennedy saa 1:35 usiku na abiria wakiwa tayari wameingia ndani ya ndege hiyo tayari kwa safari, ndipo ujumbe huo ulipoonekana saa 1:05, dakika 25 kabla ya ndege kuruka.
Abiria wote 49 walikuwa salama na upekuzi ulifanywa upya kwa abiria wote pamoja na mizigo yao. Hata hivyo hakuna bomu lililopatikana, na ndege hiyo iliruka saa 3:19
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni