Jana jioni mke wa Rais wa Kenya Mama
Margaret Kenyatta alishiriki mbio za marathoni za London na kumaliza
salama, huku mumewe Rais Uhuru Kenyatta akishuhudia.
Mke wa rais alikuwa akikimbia mbio hizo
katika kuchangisha fedha kwa ajili ya kampeni ya kupunguza vifo vya
mama wajawazito na watoto nchini Kenya.
Mama Margaret Kenyatta anaweza akaingia
kwenye rekodi za kitabu cha Guinness kwa kuwa mke wa kwanza wa rais
kuwahi kukimbia mbio hizo na kumaliza kilomita zote 42.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni